- Kundi la wanawake liliamua kuanza kutengeneza sabuni na vitakasa mikono wakitumia samadi ya ndovu na nta ya nyuki janga la COVID-19 lilipotua nchini
- Wao husaka samadi ya ndovu katika Hifadhi ya Nashulai Maasai ambayo inapakana na Mbuga ya Kitaifa ya Wanyamapori ya Maasai Mara
- John Pesi ambaye n mhudumu katika hifadhi hiyo alisema wateja hufurahia namna hutoa povu haraka na harufu yake
Habari Nyngine: Milionea Gathuo Gichuru Ageuka Mchuuzi wa Nguo Baada ya Siasa Kumfilisisha
Mara ya mwisho kusikia bidhaa inayotengenezwa kutoka kwa samadi ya ndovu ni wakati mwanasayansi wa Afrika Kusini alitengeneza pombe.
Lakini huenda tulikuwa na dhana potovu huku bidhaa nyingine yenye faida kwa binadamu kutoka kwa samadi ya ndovu sasa ikitengenezwa Kenya.
Kwa mujibu wa ripoti ya Nation, mavi ya ndovu ndio nyenzo kuu katika kutengeza sabauni ambayo wanawake 50 katika kijiji cha Sikinani, kaunti ya Narok Magharibu wanatumia kutengeneza sabuni.
Waliamua kujitafutia kipato kwa njia mpya baada ya biashara yao ya shanga kuathirika kufuatia mlipuko wa janga la COVID-19.
"Wakati wa COVID-19 tulikuwa tunakaa nyumbani bila kazi kwa hivyo tulijipata tukifanya miradi ya kuunda sabuni na vitakasa mikono tukitumia samadi ya ndovu na nta ya nyuki," alieleza mmoja wa vijana wa mradi huo.
Vijana ambao wanahusika kwenye mradi huo husaka samadi hiyo katika Hifadhi ya Nashulai Maasai ambayo inapakana na Mbuga ya Kitaifa ya Wanyamapori ya Maasai Mara.
Samadi hiyo hukaushwa na kusagwa kabla ya kutumika kuunda sabuni.
Kisha huchanganywa na mafuta ya olive, pamoja na poda kama alivyoeleza mtaalam Benard Ronoh, na kuifanya kuwa sabuni ya maji.
Kabla ya kupelekwa sokoni, sabuni hiyo hugandishwa na kukatwa vipande hitajika kisha kupigwa chapa.
Sabuni hiyo huuzwa pakiti ya gramu 50 kwa KSh 500, na wateja ambao wameijaribu akiwemo Ol Darpoi mhudumu Mara Camp alisema ni bidhaa bora.
Wateja hufurahia namna sabuni hiyo hutoa povu haraka na harufu yake ya kipekee.
Kwa sasa sabuni hizo zinasambazwa katika hoteli na kambi zilizoko Maasai Mara.
Kando na kutumika nyumbani, wanawake hao huuza bidhaa hiyo katika masoko ya Sikinani na Talek Trading Centers.
Afisa Mkuu Mtendaji wa Hifadhi hiyo, Nelson Ole Reyia, alisema mradi huo ulichochewa na jamii ya Masaai kutumia samaadi ya ndovu kuponya magonjwa ya ngozi.
READ ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.