Raia 26 wa Uganda wamefungua Kesi Nchini Ufaransa wakidai utekelezaji wa mradi huo (EACOP) kutoka Hoima, Uganda hadi Tanga umesababisha Madhara na umekiuka Haki za Binadamu ikiwemo Haki ya kumiliki Ardhi na Chakula.
Malalamiko mengine ni baadhi ya vijiji kukumbwa na mafuriko yaliyosababishwa utafutaji wa machimbo 419 ya Mafuta, Walalamikaji kupewa Vitisho, Kunyanyaswa na Kukamatwa kwa kukosoa mradi huo.
Januari 2023, Serikali ya Uganda ilitoa kibali kwa EACOP kuendeleza Mradi huo ambao Total Energies wana 62% ya hisa, CNOOC Uganda (8%), Kampuni ya Taifa ya Mafuta Uganda (UNOC) (15%), na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) (15%).