Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wananchi wa Burkina Faso waandamana dhidi ya Ufaransa

FFEF4B62 6FB3 4828 9441 7B5D913F1EF7.jpeg Wananchi wa Burkina Faso waandamana dhidi ya Ufaransa

Sun, 22 Jan 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mamia ya wananchi wa Burkina Faso wamejitokeza mabarabarani katika mji mkuu Ouagadougou kushiriki maandamano dhidi ya Ufaransa, hatua inayoonesha jinsi ushawishi wa Paris katika nchi za bara la Afrika unavyoendelea kupungua.

Hayo yameripotiwa na shirika la habari la Reuters ambalo limeeleza kuwa, waandamanaji hao wa Burkina Faso wanaituhumu Paris kuwa inaingilia masuala ya ndani ya nchi hiyo na kufanya ukoloni mamboleo.

Moja ya mabango yaliyokuwa yamebebwa na waandamanaji hao mjini Ouagadougou jana Ijumaa lilikuwa limeandikwa "Ufaransa lazima iondoke.'

Aidha waandamanaji hao huku wakipiga nara wamesema Paris imeshindwa kutekeleza ahadi na majukumu yake katika mapambano dhidi ya makundi ya wanamgambo na ya kigaidi.

Burkina Faso ni koloni la zamani la Ufaransa, na kiongozi wa kijeshi wa nchi hiyo, Ibrahim Traoré amekuwa akieleza wazi hisia zake dhidi ya Wafaransa tangu aingie madarakani, na amepanua uhusiano na nchi nyingine, ikiwa ni pamoja na Russia.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live