Taarifa kutoka nchini Niger zinaarifu kuwa baadhi ya wanajeshi wamezingira ikulu ya rais.
Upatikanaji wa wizara kadhaa katika eneo moja la mji mkuu, Niamey, pia imezingirwa.
Hakuna risasi zilizofyatuliwa na kwa wakati huu haijabainika ikiwa hili lilikuwa jaribio la wanajeshi kutoka kwa walinzi wa rais kutaka kunyakua mamlaka.
Baadhi ya vyanzo vinasema Rais Mohamed Bazoum amekuwa katika mazungumzo na wanajeshi hao.
Niger ni nyumbani kwa waasi wawili wa kijihadi.
Ni mshirika mkuu wa nchi kadhaa za Magharibi zikiwemo Ufaransa na Marekani - katika mapambano dhidi ya wanamgambo wa Kiislamu katika Afrika Magharibi.