Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wanajeshi sita wa Nigeria wauawa katika shambulizi la kuvizia

Wanajeshi Sita Wa Nigeria Wauawa Katika Shambulizi La Kuvizia Wanajeshi sita wa Nigeria wauawa katika shambulizi la kuvizia

Mon, 22 Apr 2024 Chanzo: Bbc

Jeshi la Nigeria linasema wanajeshi sita wameuawa na wanamgambo katikati mwa Jimbo la Niger.

Wanajumuisha maafisa wakuu wawili na wafanyikazi wengine wanne.

Uthibitisho huo ulitolewa siku mbili baada ya shambulizi dhidi ya timu ya doria iliyokuwa eneo ambalo majambazi wanaendesha shughuli zao katika eneo la Kati la Nigeria.

Wanajeshi hao waliripotiwa kupigwa risasi na kufariki katika shambulizi la kuvizia walipokuwa wakiitikia wito baada ya kupigiwa simu ya kuomba msaada Ijumaa usiku.

Taarifa za ndani zinasema afisa mmoja wao pia alitekwa nyara, lakini jeshi halijathibitisha hilo.

Katika taarifa yake, msemaji wa jeshi Jenerali Onyema Nwachukwu alisema wanajeshi hao waliwaua washambuliaji kadhaa na kukamata baadhi ya vifaa vyao.

Haijabainika ni nani aliyetekeleza shambulizi hilo. Nigeria na baadhi ya majirani zake wanaendelea kukabiliana na mashambulizi mabaya ya wanajihadi.

Pia inakabiliwa na unyanyasaji mkubwa wa majambazi ambao hujihusisha na utekaji nyara ili kupata fidia.

Shambulizi la hivi punde lilitokea wakati Nigeria ikijiandaa kuandaa mkutano wa kilele wa ngazi ya juu wa Afrika dhidi ya ugaidi mjini Abuja.

Chanzo: Bbc