Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Walliokuwa mawaziri Kenya wamshukuru Rais Ruto baada ya kufutwa kazi

William Ruto 2 1140x640.jpeg Walliokuwa mawaziri Kenya wamshukuru Rais Ruto baada ya kufutwa kazi

Fri, 12 Jul 2024 Chanzo: Bbc

Waliokuwa mawaziri katika baraza la mawaziri la Rais wa kenya William Ruto lililovujwa Jumanne wamekuwa wakielezea hisia zao kwenye mtandao wa kijamii wa X (zamani ikiitwa Twitter).

‘’Kwa karibu miezi 20, nimekuwa na uzoefu wa kutimiza na wenye utajiri mkubwa nikihudumu kama Katibu wa Baraza la Mawaziri la moja ya sekta muhimu zaidi nchini Kenya - Elimu. Napenda kumshukuru Rais kwa kuniamini kwa heshima hii, na nina ninamshukuru kwa hatua zote kubwa tulizozipata ndani ya muda mfupi kama huu kwani tulitoa elimu kwa watoto wetu’’ , aliandika mwenye ukurasa wake wa X aliyekuwa Waziri wa elimu Ezekiel Machogu.

Alyekuwa waziri wa michezo Ababu Namwamba pia aliandika :''Ni heshima maalum, heshima na baraka kutumikia taifa la mtu, zaidi katika Baraza la Mawaziri, chombo cha juu zaidi cha kutengeneza sera nchini. Namshukuru Mheshimiwa Rais @WilliamsRuto

kwa imani na aliyokuwa aliyooonyesha kwa uteuzi wangu kuhudumu katika Baraza la Mawaziri kwa mara ya pili katika maisha yangu ya utumishi wa umma. Mungu ibariki Kenya na kumpa Rais neema na hekima ya kuendesha nchi yetu katika bandari salama.''

Waliokuwa mawaWote wamemshukuru Bw Ruto kwa kuwapatia fursa ya kuhudumia Wakenya na taifa.

Ujumbe kwa rais kutoka kwa waliokuwa mawaziri kwa ujumla ulikuwa wa kumshukuru Bw Ruto kwa kuwapatia fursa ya kuhudumia Wakenya na taifa.

Rais huyo wa kenya alilivunja baraza lake la mawaziri na kuziacha nafasi mbili pekee-ya Kiongozi wa mawaziri na Waziri wa Masuala ya Kigeni Musalia Mudavadi na ofisi ya naibu wa rais Rigathi Gachagua .

Alisema atachukua muda kufanya majadiliano ya kuunda baraza jipya la mawaziri litakalohusika na uendeshaji wa serikali.

Hatua ya Rais Ruto ya kulivunja baraza lake la mawaziri imefuatia shinikizo kubwa la vuguvugu la vijana wa nchi hiyo linaloitwa Gen-Z lililofanya maandamano yaliyosababisha vifo na majeruhi

Chanzo: Bbc