Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Waliotibua mkutano wa Rais Ruto wasakwa

Waliotibua Mkutano Wa Rais Ruto Wasakwa Waliotibua mkutano wa Rais Ruto wasakwa

Mon, 18 Mar 2024 Chanzo: Bbc

Mamlaka nchini Kenya imeanzisha msako mkali dhidi ya watu waliotatiza mikutano ya kisiasa ya Rais William Ruto magharibi mwa nchi hiyo mwishoni mwa juma.

Ilifuatia visa viwili ambapo wavamizi walikatiza mikutano ya Rais Ruto katika kaunti za Bomet na Kericho.

Rais alikuwa katika eneo la Bonde la Ufa, ngome yake ya kisiasa, kuzindua miradi kadhaa mikutano yake ilipotatizwa huku mizozo ya kisiasa inayowakabili viongozi wa eneo hilo ikipamba moto.

Rais huyo aliyekasirishwa sana alisema viongozi wanaoshabikia machafuko kama hayo wanaathiri miradi ya maendeleo katika eneo hilo, akitaja usumbufu huo kuwa "upumbavu".

Waziri wa Mambo ya Ndani Kithure Kindiki Jumatatu aliagiza polisi kuwakamata mara moja watu waliohusika na matukio hayo.

Waziri huyo alikutana na wakuu wa usalama wa eneo hilo na kuwapa jukumu la "kuhitimisha uchunguzi na kuwakamata waandaaji, wafadhili na wahusika wa uhuni".

Chanzo: Bbc