Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Waliosambaza picha feki za utupu za Rais wa Zimbabwe waachiwa

13466 Zimbabwe+pic Waliosambaza picha feki za utupu za Rais wa Zimbabwe waachiwa

Thu, 11 Nov 2021 Chanzo: BBC

Wanandoa wa Zimbabwe wameachiliwa huru kutoka kizuizini baada ya hakimu kufutilia mbali kesi dhidi yao kwa madai ya kusambaza picha bandia za utupuza rais wa taifa hilokatika mtandao wa WhatsApp, amesema wakili wao.



Sarudzayi Ambiri Jani, 39, na Remember Ncube, 35, walihukumiwa kifungo Juni 2020 kwa madai ya kuhujumuna kumtusi rais lakini hakufunguliwa mashtaka.

Picha hizo bandia zilionekana kumuonesha rais Emmerson Mnangagwaakiwa utupu , huku akiwa amezibwa na kitambaa kidogo cha bendera ya Zanu-PFna barakoa ambayo ilikuwa imeficha sehemu zake za siri.

Hakimu Takudzwa Gwazemba, aliwaachilia huru wawili hao kutoka kizuizini kwasababu upande wa mashtaka ulikuwa umeshindwa kuwafungulia mashtaka mwaka mmoja baada ya kukamatwa.

Chanzo: BBC