Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Waliopindua Serikali ya Niger wakubali kuzungumza na Putin

Urusi 'haijafungia Milango' Kampuni Za Kigeni   Putin Waliopindua Serikali ya Niger wakubali kuzungumza na Putin

Wed, 16 Aug 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mkutano wa kijeshi wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS) utafanyika Alhamisi Agosti 17 na Ijumaa Agosti 18 nchini Ghana, kujadili uwezekano wa kuingilia kijeshi nchini Niger na kumrejesha mamlakani rais Mohamed Bazoum ambaye alitimuliwa kupitia mapinduzi ya kijeshi.

Wakati huo huo, Urusi na Mali zimetoa wito Jumanne, Agosti 15, kupitia sauti ya marais wao, kusuluhisha mgogoro huo “kwa njia ya amani ya kisiasa na kidiplomasia”

Mazungumzo haya ya simu kati ya Moscow na Bamako yamefanyika “kwa juhudi za Mali”, imebainisha huduma ya vyombo vya habari ya Kremlin.

Katika taarifa, ikulu ya Kremlin imebaini kwaba marais wa Urusi Vladimir Putin na Mali Assimi Goïta “wamesisitiza umuhimu wa kutatua hali kuhusu Jamhuri ya Niger kwa njia ya amani ya kisiasa na kidiplomasia”.

Saa chache baadaye, katika mkutano wa 11 wa usalama wa kimataifa kuhusu Moscow mkutano ulioandaliwa na jeshi la Urusi  Waziri wa Ulinzi wa Mali ameonyesha msimamo wako.

Bila kutaja jina, lakini kwa matamshi ya uwazi, Sadio Camara ameikosoa vikali ECOWAS.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live