Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Walinzi mpaka wa Saudia wawaua mamia ya Waethiopia - Human Rights Watch

Ef545115 49ec 4173 Be40 5fcd2323f91a Walinzi mpaka wa Saudia wawaua mamia ya Waethiopia - Human Rights Watch

Mon, 21 Aug 2023 Chanzo: Bbc

Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limewashutumu walinzi wa mpakani wa Saudi Arabia kwa kuwaua mamia ya wahamiaji wa kiuchumi wa Ethiopia waliokuwa wakijaribu kuvuka kutoka Yemen yenye vita.

Wanasema takribani watu 655 wameuawa na walinzi tangu mapema mwaka jana.

Baadhi walipigwa risasi, wengine kuuawa au kulemazwa na silaha za vilipuzi.

Shirika hilo lilitumia miezi kadhaa kukusanya ushahidi, baada ya Umoja wa Mataifa kutoa madai kama hayo mwaka jana.

Human Rights Watch imeyataja mauaji hayo kuwa yameenea na ya kimfumo, na yanasema yanaweza kuwa uhalifu dhidi ya ubinadamu.

Mwezi Machi, serikali ya Saudia ilikataa kabisa pendekezo lolote kwamba vikosi vyake vilihusika katika mauaji ya kuvuka mpaka.

Chanzo: Bbc