Mon, 25 Jul 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wakimbizi 17 wa Haiti wamefariki Dunia baada ya mashua waliyokuwa wakiitumia kuzama kwenye maji huku wengine wengi wakiwa hawajulikani walipo.
Walikuwa njiani kuelekea Miami Nchini Marekani kupitia Bahamas, sababu ya kukimbia Nchi yao zikitajwa kuwa ni umasikini na vurugu za wahalifu.
Kikosi cha waokoaji kimesema kimefanikiwa kupata miili 17 akiwemo mtoto mchanga huku Watu 25 wakiokolewa kati yao Wanawake wakiwa ni wanne na inadaiwa mashua hiyo ilibeba watu 60
Chanzo: www.tanzaniaweb.live