Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wakili Ombeta asema yuko tayari kumwakilisha jamaa aliyempiga Rais Macron kofi

762267cfeb87d490 Wakili Ombeta asema yuko tayari kumwakilisha jamaa aliyempiga Rais Macron kofi

Wed, 9 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Kisa hicho kilitokea wakati Macron alikuwa ametembelea eneo la Drome kusini mashariki mwa Ufaransa ambapo alikuana na wahudumu wa hoteli na wanafunzi

- Tukio hilo la Jumanne, Juni 8, liliwacha wengi vinywa wazi wakijaribu kujiuliza hatua ambayo rais huyo atachukuwa dhidi ya jamaa aliyemzaba kofi

- Wakili Mkenya Cliff Ombeta sasa anasema anatafuta visa kusafiri kuelekea Ufaransa ili kumwakilisha jamaa huyo

Wakili maarufu nchini Cliff Ombeta amesema yuko tayari kumwakilisha jamaa ambaye alimpiga kofi Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron wakati wa mkutano wa hadhara.

Huku akitoa kauli yake kuhusu video iliyopakiwa na mcheshi Churchill ikimuonyesha raia akimzaba kofi Macron usoni wakati alitoa mkono kumsalimu, Ombeta alisema anatafuta visa kusafiri kuelekea Ufaransa ili kumwakilisha kortini.

"Cliff Ombeta anahitajika haraka Ufaransa.... mtu amegeuza maski ya rais," Churchill alitania huku Ombeta akijibu na kusema: "Ni visa ndio najaribu kupata kaka"

Kauli ya Ombeta iliwatekenya wanamtandao kwenye Twitter wakitoa maoni yao ya namna wakili wa Mahakama Kuu atamtetea jamaa huyo.

@jesang: "Uso wa rais kwa bahati mbaya ulikutana na mkono wa raia wa kawaida"

@alouispierry: "Cliff akifungua: Rais aliweka uso wake kwenye mkono wa mteja akifanya zoezi lake la kila siku."

@joemulwa11: "Inanonekana unawafunz ahadi watu wa nje."

Kisa hicho kilitokea wakati Macron alikuwa ametembelea eneo la Drome kusini mashariki mwa Ufaransa ambapo alikuana na wahudumu wa hoteli na wanafunzi.

Alikuwa ametoa mkono wake kumsalimu jamaa huyo ambaye aligeuka na kumzaba kofi kiongozi wa taifa.

Tukio hilo la Jumanne, Juni 8, liliwacha wengi vinywa wazi wakijaribu kujiuliza hatua ambayo rais huyo atachukuwa dhidi ya jamaa aliyemzaba kofi.

Walinzi wa Macron waliingilia haraka na kumsukuma jamaa huyo na kisha kumpeleka Macron mahali salama.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke