Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wakenya wanateseka kwa sababu ya kukataa kumchagua Raila, Mbunge Kaluma asema

D8538acdf1135cd2 Wakenya wanateseka kwa sababu ya kukataa kumchagua Raila, Mbunge Kaluma asema

Wed, 14 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Kulingana na EPRA, itaongeza bei ya petroli kwa KSh 4.30,huku ya dizeli ikipanda kwa KSh 2.30 kuanzia Jumatano, Aprili 14, saa sita usiku

- Bei ya petroli jijini Nairobi kwa hivyo itakuwa inauzwa KSh 127.11 lita moja, huku dizeli ikiuzwa KSh 109.96 kwa kila lita

- Kaluma alisema Wakenya wanavuna kile walichopanda baada ya kukataa kumchagua Raila Odinga kama rais

Mbunge wa Homa Bay Mjini, Peter Kaluma amewalaumu Wakenya kuwa chanzo cha kuongezeka kwa bei ya mafuta ambayo imechangia gharama ya maisha kupanda.

Katika taarifa kwenye kitandazi chake cha Twitter, mwanachama huyo wa Orange Democratic Movement (ODM) alihoji kuwa Wakenya wanateseka kwa sababu ya kufanya uamuzi mbaya wakati wa chaguzi za mwaka 2017.

Kaluma alisema Wakenya wanavuna kile walichopanda baada ya kukataa kumchagua Raila Odinga kama rais.

"Tunashukuru wale ambao walimkataa Raila Odinga na kupigia kura serikali ya sasa Tuvumilie kuwa WaKenya. Tuko Pamoja hadi mwishi," aliandika.

Mbunge huyo alikashifu ushuru ghali unaotuzwa bidhaa za mafuta nchini ambayo ni ya juu ikilinganishwa na mataifa mengine ya Afrika Mashariki.

"Ushuru unaotozwa bidhaa za mafuta ni nusu ya gharama yake. Uganda na Rwanda wanauza mafuta bei nafuu licha ya kuagiza nje kupitia Kenya, hata ukiongezea gharama ya usafirishaji. Hakuna taifa hutajirika kutokana na ushuru ghali!" aliongezea.

Matamshi ya Kaluma yanakujia baada ya Mamlaka ya Kudhibiti Biashara za Mafuta na Kawi (EPRA) kupandisha bei ya mafuta.

Kulingana na EPRA, itaongeza bei ya petroli kwa KSh 4.30,huku ya dizeli ikipanda kwa KSh 2.30 kuanzia Jumatano, Aprili 14, saa sita usiku.

Bei ya petroli jijini Nairobi kwa hivyo itakuwa inauzwa KSh 127.11 lita moja, huku dizeli ikiuzwa KSh 109.96 kwa kila lita.

Mamlaka hiyo ilisema bei hiyo imeongezeka kutokana na ongezeko la bei ya soko ya kimataifa kupanda hadi KSh 6,990 Aprili kutoka kwa KSh 6,500 ya mnamo Machi.

Rais Uhuru Kenyatta alimlambisha sakafu Raila kwenye uchaguzi wa mwaka 2017 baada ya kupata 54% ya kura zilizopigwa.

Hata hivyo, ushindi huo ulibatilishwa na Mahakama ya Upeo kwa msingi wa udanganyifu baada ya Raila kuwasilisha kesi ya kupinga matokeo hayo.

Kiongozi huyo wa ODM alikataa kushiriki marudio ya uchaguzi huo akisema ana shauku na Tume ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC).

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke