Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wakenya wampongeza Rais Uhuru Kenyatta kwa kuondoa "Kafyu"

B9260667d6801c2b Wakenya wampongeza Rais Uhuru Kenyatta kwa kuondoa "Kafyu"

Wed, 20 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Wakenya kupitia mitandao ya kijamiii wamesherehekea baada ya Rais Uhuru Kenyatta kutangaza kuondolewa kwa kafyu ya kutokuwa nje kutoka saa nne usiku hadi saa kumi alfajiri.

Kafyu imekuwepo tangu mwezi Machi 2020 wakati ambapo maradhi ya Covid-19 yalichipuka nchini Wakenya walitakiwa kutokuwa nje usiku kuanzia majira ya saa nne usiku hadi saa kumi Alfajiri.

Uhuru amesema amefanya uamuzi wa kuondoa kafyu baada ya kufanya mashauriano na Wizara ya Afya

Kafyu hiyo iliwekwa kwa mara ya kwanza mwezi Machi 2020 ikiwa ni mojawapo ya njia za kudhibiti na kuzua msambao wa virusi vya COVID- 19 ambavyo viliathiri ulimwengu mzima.

Akihutubia taifa akiwa katika sherehe za Mashujaa Day katika uwanja wa Wang'uru kaunti ya Kirinyaga siku ya Jumatano, Oktoba 20, Uhuru alisema masharti hayo kwa sasa hayatafuatwa.

" Kulingana na mamlaka ninayo kama Rais, ninaagiza kuondolewa mara moja kwa kafyu ya kutoka saa nne usiku hadi saa kumi asubuhi ambayo imekuwepo tangu mwezi Machi mwaka wa 2020, " Alisema Rais huku akishangiliwa na Wakenya waliohudhuria sherehe ya Mashujaa. Kirinyaga.

Wakenya wameelezea furaha yao na TUKO.co.ke iliweza kuangazia baadhi ya maoni;





Aidha, inaaminika kwamba maeneo ya burudani ambayo hupiga sherehe usiku yaliaminika kuchangia pakubwa katika kusambaa kwa virusi vya Covid-19 na hivyo kafyu kuwekwa ili kudhibiti msambao.

Wakati huo huo, Uhuru alisema kwamba idadi ya waumini kanisani iongezwe kutoka theluji moja hadi theluji mbili ila masharti ya wizara ya afya yaendelee kuzingatiwa.

Uhuru aliongezea kwamba zaidi ya watu milioni tano wamechanjwa dhidi ya virusi vya Covid-19 na bado serikali inalenga kuchanja watu milioni 10.

" Leo nafurahia kutangazia taifa kwamba tunakaribia kufikia malengo yetu, kufikia sasa tumeweza kuwachanja watu milioni tano, lazima tufikishe milioni kumi," Alisema Rais.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke