Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wakenya wamhoji IG Mutyambai kuhusu maafisa wake kula hongo

3b8ea028682205ab Wakenya wamhoji IG Mutyambai kuhusu maafisa wake kula hongo

Tue, 13 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Inspekta Jenerali wa Polisi Hillary Mutyambai amewataka Wakenya waripoti visa vyovyote vya ufisadi katika vituo vyovyote vilivyo karibu

- Kumekuwa na tetesi kwamba baadhi ya wananchi wanatoa hongo kwa maafisa wa polisi ndiposa waruhusiwe kusafiri nje ya kaunti zilizofungwa kwa ajili ya kudhibiti maambukizi ya covid-19

- Jumatatu wiki hii wizara ya Afya iliripoti kuwepo kwa maambukizi 486 baada ya sampo 2989 kufanyiwa vipimo

- Hali hii ilipelekea Mkenya mmoja kumuuliza Mutyambai sababu ya maafisa wake kuwaruhusu wananchi kuvuka kwenda na kuingia katik kaunti ambazo zilifungwa

Inspekta Jenerali wa polisi Hillary Mutyambai amekabiliwa na maswali chungu nzima kwenye mtandao wa Twitter baada ya tetesi kuibuka kwamba maafisa wake wamekuwa wakichukua hongo.

Wakenya wametilia shaka iwapo kama kweli masharti yaliowekwa na Rais Uhuru Kenyatta ikiwemo ya kufunga kaunti tano kwa ajili ya kudhibiti maambukizi ya virusi vya COVID-19 yanafuatwa.

Imeripotiwa kwamba baadhi ya wakenya wamekuwa wakilazimika Kutoa Kitu Kidogo, (KKK) ili waruhusiwe kuondoka na kuingia kaunti zilizofungwa.

Akiwa mwenye ghadhabu Mkenya mmoja mwenye akaunti @krazygb alidai kwamba ufisadi umejaa Kenya sana huku akifichua jinsi baadhi ya waelekezaji wa watalii wamekuwa wakitumia hongo ili kupita katika vizuizi vya polisi.

" Mbona baadhi ya waelekezaji wa watalii wasioruhusiwa kupita vizuizi wanatumia hongo kupitisha watalii, ilhali waliopewa leseni wanazuiwa kupita, mbona wasipewe wote leseni bila ubaguzi?." Alisema Mkenya huyo.



Akijibu madai hayo, Mutyambai alisema kwamba hakuna anayeruhusiwa kupita vizuizi isipokuwa Wakeeny wenye kutoa huduma muhimu.

"Tafadhali toa ripoti ya visa vya ufisadi katika kituo cha polisi kilicho karibu nawe. Ushahidi utahitajika ili kusaidiwa kwa haraka. Hakuna anayeruhusiwa kutoka katika kaunti zilizofungwa isipokuwa watoaji huduma muhimu." Alisema Mutyambai.

Aidha, Mutyambai aliwashukuru Wakenya waliomhoji na kusema waendelea vivyo kwa ajili ya kukabiliana na ufisadi.

"Asanteni sana kwa kujiunga na #EngageTheIG, kuna mambo ambayo tunashughulikia faraghani na hii ni kwa ajili yenyu." Alisema Mutyambai.

Read: ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke