Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wakenya wakimbilia mikopo ya serikali saa chache baada ya kuzinduliwa

Wakenya Wakimbilia Mikopo Ya Serikali Saa Chache Baada Ya Kuzinduliwa Wakenya wakimbilia mikopo ya serikali saa chache baada ya kuzinduliwa

Thu, 1 Dec 2022 Chanzo: Bbc

Zaidi ya Wakenya milioni moja wamejiandikisha kwa mpango wa mikopo ya serikali inayolenga vijana na wafanyabiashara wasio rasmi siku moja tu baada ya kuzinduliwa.

Mpango huo, unaojulikana kama Hustler Fund, ulizinduliwa na Rais William Ruto Jumatano na tayari ametoa zaidi ya shilingi 400m ($3.3m; £2.7m) kwa wakopaji.

Vyombo vya habari vya ndani vilimnukuu waziri wa vyama vya ushirika akitoa mfano wa kuchukuliwa kwa mikopo hiyo, na hadi miamala 600 kwa sekunde, saa baada ya uzinduzi - ambao ulipungua baadaye.

Wakopaji wanaweza kupata pesa kwa kupiga nambari ya USSD au kutumia programu kwenye simu zao za rununu.

Mikopo hiyo inaanzia kati ya $4 (£3) na $408 kwa wakopaji binafsi. Mikopo kwa vikundi na biashara ndogo itazinduliwa baadaye.

Wakopaji wanatarajiwa kurejesha mkopo ndani ya siku 14, na riba ya kila mwaka ya 8% iliyohesabiwa kwa siku itatozwa.

Hazina hiyo ilikuwa ahadi kuu ya kampeni na rais aliyeingia madarakani mwezi Septemba.

Ameupigia debe mfuko huo unaolenga zaidi ya watu milioni nane kuwa ndio utakaotoa maisha kwa vijana, wanawake na makundi ya watu wa kipato cha chini ambao hawawezi kupata mikopo kutoka kwa wakopeshaji wa kibiashara.

Chanzo: Bbc