Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wakenya Wavamia IMF Wakilaumu Nchi Yao Kukopeshwa

IMF2?fit=1024%2C576&ssl=1 Wakenya Wavamia IMF Wakilaumu Nchi Yao Kukopeshwa

Sun, 25 Apr 2021 Chanzo: globalpublishers.co.tz

Kwa mara ya pili wiki hii, mtandao wa kijamii wa shirika la fedha duniani IMF umejipata ukivamiwa na ukosoaji kutoka kwa Wakenya,wanaolilaumu kwa kuendelea kuikopesha fedha nchi yao.

Matangazo mubashara ya ukurasa wa Facebook ya IMF yalijazwa na maoni ya Wakenya ambao hawataki madeni Zaidi yatolewe kwa serikali, wengi wao wakisema pesa nyingi zitafanyiwa ubadhilifu na maafisa wa taifa lao.

Katika maoni yao, baadhi walielezea hofu kuhusumadeni ya umma ambayo yamefikia hadi dola bilioni 70 mwishoni mwa mwaka 2020.

Matangazo hayo yaliongozwa na Kristalina Georgieva MkurugenziMkuu wa IMF Alhamisi usiku yaliyomalizika baada ya dakika 23.

Chanzo: globalpublishers.co.tz