Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wakenya Wakabili Polisi Waliofunga Thika Road Baada ya Kafyu Kufika

0714b008886baf65 Wakenya Wakabili Polisi Waliofunga Thika Road Baada ya Kafyu Kufika

Sun, 18 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Polisi walidaiwa kuchukua fungua za baadhi ya magari na kusema itabidi wote waliochelewa kulala kwenye magari yao hadi saa kumi asubuhi

-Vuta nivute ilishuhudiwa kwa muda kabla ya baadhi ya waliofungiwa kuamua kuwashinikiza polisi kufungua barabara hiyo

- Ni hali ambayo imezua mjadala mkali mtandaoni wengi wakitaka Rais Uhuru kuskia kilio cha watu wake

Wakazi wa Nairobi waliokuwa wamechelewa nje na masaa ya kafyu kufika walijipata pabaya baada ya polisi kufunga barabara ya Thika Road.

Polisi waliokuwa katika kizuizi walisema waliokuwa wamechelewa watalazimika kulala kwenye magari yao barabarani.

Ni hatua iliyozua msongamano mkubwa wa magari kwenye barabara hiyo huku waliofungiwa wakiteta kuhusu ukatili wa polisi na serikali wanayohudumia.

Baada ya muda wa majibizano, wakazi hao walilazimu polisi hao kuondoa kizuizi hicho ili waendelee na safari.



Kulingana na video iliyochapishwa na jasusi wa kibinafsi Jane Mugoh, Wakenya wanaonekana wamekwama kwenye msongamano huku wengi wakimlilia Rais Uhruu Kenyatta kuwa na huruma kwa Wakenya.

Mugo anashangaa ni kwa nini hata ambulensi iliyo na mgonjwa ilizuiwa kupita na hivyo kuhatarisha maisha yake.

Tukio hilo lilizua hisia mseto kwenye mitandao huku baadhi ya Wakenya wakisema Rais anafaa kufungua nchi sasa.

Rais Uhuru Kenyatta alitoa sheria mpya za kukabiliana na maambukizi ya Covid-19 ikiwamo kafyu ya kutokuwa nje kuanzia saa mbili usiku katika kaunti tano ambazo alisema zinaongoza katika maambukizi.

Kaunti hizo zilizofungwa mipaka yake pamoja na masaa ya kafyu kuongezwa kuanzia saa mbili hadi saa kumi asubuhi ni Nakuru, Nairobi, Kiambu, Kajiado na Machakos.

Mbunge Sylvanus Osoro alisema wakati umefika kwa rais kukubali sheria hizi kali za kukabili Covid-19 zinaumiza Wakenya pakubwa na hivyo kuziondoa.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke