Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wahusika kifo cha Rais wapandishwa kizimbani

687f3a0f A97d 4abd B052 B4b60b02600c W1200 R1 1140x640 Wahusika kifo cha Rais wapandishwa kizimbani

Tue, 14 Feb 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mamlaka za Usalama nchini Chad, zitaanza kuwasikiliza waasi 150 wanaotuhumiwa kusababisha kifo cha Rais Idriss Déby, katika Gereza la Kléssoum, lenye ulinzi mkali, ambao wanashtakiwa kwa ugaidi, kuandikisha watoto askari, utumwa, kudhoofisha usalama wa serikali, na mauaji ya rais.

Washukiwa hao ni kutoka chama cha Front for Concord and Change in Chad (FACT), lenye vuguvugu la waasi ambalo lilianzisha mashambulizi ya kuipindua serikali ya Chad kutoka kambi zake za nyuma nchini Libya mwaka 2021.

Idriss Deby, aliuawa kwenye mstari wa mbele mwezi Aprili 2021 wakati akisimamia operesheni za jeshi kuwarudisha nyuma waasi na alikuwa ametoka kushinda mamlaka mpya katika kura iliyoshutumiwa kuwa ya ulaghai.

Kwa msaada wa Ufaransa, watawala wapya wa kijeshi wa Chad waliweza kuwazuia waasi kusonga mbele, na takriban miaka miwili tangu kifo cha Deby, mazungumzo kati ya vuguvugu la waasi na serikali ya Chad yamekwama wakitaka wanachama wake waachiliwe huru.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live