Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wahome aachiliwa kwa dhamana Kenya

Wahome Aachiliwa Kwa Dhamana Kenya Wahome aachiliwa kwa dhamana Kenya

Fri, 31 Mar 2023 Chanzo: Voa

Mahakama ya Kenya siku ya Alhamisi imemuachilia kwa dhamana dereva wa mashindano ya magari nchini humo Wahome Maxine, ambaye amekuwa chini ya ulinzi wa polisi kwa tuhuma za mauaji.

Wahome, mwenye umri wa miaka 27, anadaiwa kumshambulia mpenzi wake na dereva mwenzake Asad Khan aliyekuwa na umri wa miaka 50 katika nyumba yao iliyoko katika mji mkuu wa Nairobi Desemba mwaka jana.

Khan alifariki dunia kutokana na majeraha kwenye kifundo cha mguu wake wa kulia baada ya kukaa hospitali kwa wiki moja.

"Ninampa mtuhumiwa bondi ya shilingi milioni mbili za Kenya, na mdhamini wa kiwango kama hicho cha pesa," hakimu wa mahakama kuu Lilian Mutende alitoa maamuzi hayo, na kuongeza kuwa upande wa mwendesha mashtaka haukuwasilisha ushahidi wa kutosha ili mtuhumiwa anyimwe dhamana.

Mutende alimuamuru Wahome akabidhi hati yake ya kusafiria katika mahakama na akae mbali na mashahidi wote.

Wahome, ambaye alijipatia umaarufu kwa kuwa mwanamke wa kwanza Mkenya kushinda mbio za magari daraja la tatu za WRC Safari Rally mwezi Juni mwaka jana, Wahome alikana makosa.

Mwezi huu aliondolewa kwenye programu ya WRC Young Rally Stars.

Chanzo: Voa