Serikali ya Malawi imesitisha utoaji wa hati za kusafiria kufuatia uhalifu wa kimtandao uliofanywa kwenye kompyuta za huduma za Idara ya Uhamiaji.
Rais Lazarus Chakwera amewaambia wabunge kwamba kulengwa kwa idara hiyo na wahalifu ni sawa na "ukiukaji mkubwa wa usalama wa taifa".
Amefichua kuwa wadukuzi hao wa siri za Uhamiaji walikuwa wakiomba fidia ili warejeshe mambo katika ukawaida wake.
Lakini rais amesema serikali haitakubali madai yao na kwamba inapambana kutatua tatizo hilo na kuwakamata.
"Hatuko katika biashara ya kuwaridhisha wahalifu kwa pesa za umma, wala hatuko katika biashara ya kufanya mazungumzo na wale wanaoshambulia nchi yetu," amesema.