Mon, 25 Jul 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Zaidi ya watu 500 wamekusanyika na kuandamana wakilalamikia gharama za maisha kuwa kubwa Jijini Kuala Lumpur Nchini Malaysia yakihusisha wanasiasa vijana wa upinzani ambapo pia walipata nafasi ya kutoa hotuba.
Sehemu ya madai ya waandamani ni kudhibiti ongezeko la bei za bidhaa, usalama wa chakula na kutoa misaada kwa Wananchi.
Maandamano hayo yalihusisha watu kutoa taasisi tofauti ambapo Polisi waliweka vizuizi na kueleza kuwa hawakuwa na taarifa juu ya maandamano hayo kama inavyotakiwa kufanyika kwa mujibu wa sheria.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live