Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wafuasi wa Ruto wamjia juu Uhuru baada ya kumtaka DP ajiuzulu

91697a2629404de9 Wafuasi wa Ruto wamsuta vikali Uhuru baada ya kumtaka DP ajiuzulu

Tue, 24 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Wandani wa Naibu Rais William Ruto wamevurumisha makombora dhidi ya Rais Uhuru baada ya kumtaka Ruto ajiuzuluWakiongozwa na Seneta Kipchumba Murkomen, wandani wa Ruto walisema Uhuru ndiye anatakiwa kuwa wa kwanza kujiuzuluWalisema hawawezi kumruhusu Ruto ajiuzulu kwa sababu anajishughulisha na kubadilisha maisha ya Wakenya kupitia mfumo wa uchumi wa bottom-up Wandani wa Naibu Rais William wamemsuta vikali Rais Uhuru Kenyatta kwa kumtaka naibu wake ajiuzulu iwapo hafurahishwi na serikali ya Jubilee.

Katika mahojiano na waandishi wa habari katika Ikulu Jumatatu, Agosti 23, Uhuru akisemekana kukerwa alisema iwapo Ruto hafurahishwi na serikali anavyodai, anatakiwa ajiuzulu.

Matamshi ya Uhuru yaliwaacha sehemu ya wanasiasa wa Tangatanga wakiwa na mate machungu mdomoni kutokana na maoni yao kwenye mitandao ya kijamii.

Wakiongozwa na Seneta wa Elgeyo Marakwet, Kipchumba Murkomen wandani wa Ruto walisema Uhuru ndiye anatakiwa kuwa wa kwanza kujiuzulu.

"Kujiuzulu kutoka ofisi ya umma si hifadhi ya mtu maalum au ofisi, hata yule mwingine anaweza kujiuzulu na Kenya itaendelea," alisema.

Read also

Rais Uhuru Amtaka William Ruto Ajiuzulu kwa Kukaidi Serikali

Kwa upande wake Seneta Mteule Millicent Omanga alitumia methali ya Kiswahili kuonyesha hisia zake dhidi ya matamshi ya Uhuru.

"Sijawahi kuelewa vyema msemo wa 'asante ya punda ni mateke' hadi leo. Ni sawa tu," alisema.

Mbunge wa Kikuyu, Kimani Ichung'wa alisema hawatamruhusu Ruto ajiuzulu kwa sababu anajishughulisha na kubadilisha maisha ya Wakenya kupitia mfumo wa uchumi wa bottom-up

"Hatuwezi kukuruhusu wewe @WilliamsRuto ujiuzulu. Tulikupigia kura sawia na tulivyomchagua Uhuru. Zingatia mfumo wa bottom-up na maisha ya watu waliokuchagua," alisema.

Hii hapa baadhi ya maoni mengine ya wanachama wa Tangatanga:



Jiuzulu kama hauna furahaUhuru akisemekana kukerwa alisema iwapo Ruto hafurahishwi na serikali anavyodai, anatakiwa ajiuzulu na kupeleka ajenda yake kwa watu.

Rais pia alisema japo hapingi azma ya Ruto kisiasa, si sawa kwake kuenda kinyume na serikali ambayo anatumikia.

Kiongozi huyo wa taifa alisema hajawahi kumzuia Ruto kufuata ndoto zake za kuwa rais lakini mbinu yake ya kupiga kampeni si sawa.



Read also

Kuanguka kwa BBI ni Baraka Kubwa kwa Rais Kenyatta, Moses Kuria asema

"Sijawahi kumzuia, yuko huru kufanya hivyo. Lakini nafikiri si vyema namna anaifanya, kwa kuenda kinyume na serikali ambayo anatumikia, nafikiri si sawa," aliongezea.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke