Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wacheni kusumbua Rais Uhuru kichwa, Ruto awaonya vinara wa NASA

09e05cc70f3bfd78 Wacheni kusumbua Rais Uhuru kichwa, Ruto awaonya vinara wa NASA

Sun, 11 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Ruto aliwasuta vinara wa NASA akiwataka kukoma kumsumbua Rais na badala yake waunganeAliwaonya kuwa iwapo wataendelea kutofautiana bila mpango, basi kikosi chake kitakuwa tayari kuingia ikulu 2022.Naibu Rais Pia alitetea sababu zake za kutoa michango kanisani akisema ni kutokana na umbali ambao Mungu amemtoa

Naibu Rais William Ruto amemkashfu kinara wa ODM Raila Odinga na vinara wengine wa NASA kwa kumvuta Rais Uhuru Kenyatta katika malumbano ya muungano wao.

Akizungumza wakati wa ibada Jumapili, Julai, 11, katika Kanisa la African Holy Ghost Christian mtaa wa Huruma, Nairobi, Ruto aliwasuta vinara wa NASA akiwataka kukoma kumsumbua Rais na badala yake waungane.

“Wote ni walafi na wanapigania faida zao binafsi. Wengine wanasema risasi na wengine wanalia eti pesa. Rais alichaguliwa kuongoza Wakenya wote si watu watano ama sita," Ruto alidai.

Ruto pia aliongezea kuwa Upinzani ulianza kumzingua Uhuru na mswada wa kurekebisha katiba na wakati uligonga mwamba wanataka sasa awasadiie washinde kura.

Read also

Kinyang'anyiro 2022: Wanasiasa Wanaotazamiwa Kumtoa Waiguru Kijasho Katika Kutetea Kiti Chake

Matumaini Kushinda Kura 2022Aliwaonya kuwa iwapo wataendelea kutofautiana bila mpango, basi kikosi chake kitakuwa tayari kuingia Ikulu 2022.

Pia alitetea sababu zake za kutoa michango kanisani akisema ni kutokana na umbali ambao Mungu amemtoa.

“Mbona uko na shida na sisi tukienda kanisani? Watu wengine hatuna warithi kando na Mungu," aliongezea.

Haya yanajiri wiki moja baada ya Ruto kumtolea makavu Raila Odinga kwa mazoea yake ya kurushia vijembe vugu vugu lake la 'hasla' na michango kanisani.

Ruto alisema alimsaidia Raila kuwa waziri mkuu na hivyo anatakiwa kuwaruhusu Wakenya wanaoishi mashinani kufaidika na michango yake.

Ruto alisema badala ya Raila kukosoa vugu vugu lake, wapinzani wake wanatakiwa kuuza sera zao kwa Wakenya.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke