Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wacha kumkataa mtoto wako, Orengo aambiwa kuhusu kupinga BBI

877acde5ae585b49 Wacha kumkataa mtoto wako, Orengo aambiwa kuhusu kupinga BBI

Mon, 3 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Baadhi ya wanachama wa ODM walikuwa wamemkashifu Seneta wa Siaya James Orengo kwa kusaliti chama hicho

- Mbunge wa Suna Mashariki Junet Mohamed alisema sasa seneta huyo anapinga BBI, licha ya kaunti yake kuwa ya kwanza kupitisha mswada huo

- Junet pia amesutwa na viongozi wanaomuegemea Orengo kwa kushindwa kutanzua utata kwenye mswada huo

Msimamo wa hivi punde wa Seneta wa Siaya, James Orengo kuhusu Mpango wa Maridhiano(BBI) umezua mgawanyiko katika Chama cha Orange Democratic Movement ( ODM).

Seneta huyo alikashifiwa hivi majuzi kwa kuimba wimbo tofauti na kiongozi wa chama hicho Raila Odinga kuhusu BBI.

Hii ni kufuatia hatua yake ya kukosa uhalali wa maeneo bunge 70 yaliyopendekezwa na BBI, jambo ambalo chama hicho kimetaja kama usaliti.

“Orengo aliongoza kamati iliyoandaa mswada wa mwisho. Hawezi kugeuka sahii na kusema hatukukubaliana. Hawezi kumtoroka mtoto wake. Anajaribu kukataa huo mswada kwa kuwa mwandishi. Hii ni usaliti wa kisiasa,”Junet Mohamed gazeti la Sunday Nation.

Junet aliwaomba wanasiasa wanaopinga BBI, hususan wa ODM kuwazia hatua ambazo mswada huo umepiga na kusema huenda wamesahau taifa hili ilipokuwa kabla ya mswada huo.

Junet pia amesutwa na viongozi wanaomuegemea Orengo kwa kushindwa kutanzua utata kwenye mswada huo uliochochewa na majemedari wa Rais Uhuru Kenyatta.

Matamshi ya Orengo yameweka taswira kuwa huenda kulikuwa na mchezo mchafu wakati mswada wa mwisho wa BBI uliandaliwa na wakati uliwasilishwa katika mabunge ya kaunti.

“Nimewaona baadhi ya watu wakinikashifu kuwa huenda niliuza ODM kwa kushindwa kusaini kila ukurasa wa mswada huo kuulinda dhidi ya kubatilishwa kwa njia yoyote lakini ilikuwa kazi ya mwenyekiti kutia saini sio mimi,” said Junet.

Hata hivyo, Orengo alisema alikuwa ana hakikisha kuwa mabadiliko ya katiba yanamshughulikia kila mtu sio watu wachache.

"Tunahakikisha kuwa mswada wa BBI unamlinda mwananchi wa kawaida. Nilisema kuwa Migori, Kisii, Busia na Homa Bay zinatakiwa kuongezewa maeneo bunge."

“Tunatakiwa kuhakikisha kuwa BBI unaguzia yaliyoko kwenye ripoti kamili,” alisema Orengo.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke