Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wabunge wanaomuunga mkono DP Ruto watia saini kumuondoa Waziri Matiang'i

Fef8fb163cd59aaa Wabunge wanaomuunga mkono DP Ruto watia saini kumuondoa Waziri Matiang'i

Fri, 8 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Wabunge hao ambao wengi wanamuunga mkono Naibu Rais William Ruto walitia saini mswada huo wa kumtimua Waziri wa Masuala ya ndani Fred Matiang'i.

Wabunge hao wamemtuhumu Matiang'i kwa utumizi mbaya wa mamlaka ikijumuisha ukiukaji wa Sura ya Sita ya Katiba Stakabadhi zilizopitiwa na TUKO.co.ke zilionyesha kwamba wabunge 92 tayari wametia saini na kuunga mkono mswada huo.

Baadhi ya Wabunge wakiongozwa naye Mbunge wa Nyali Mohamed Ali wanajianda kumngatua mamlakani Waziri wa Masuala ya Ndani Fred Matiang'i .

Mswada huo ulidhaminiwa na Mbunge wa Nyali Mohamed Ali, ambaye anatarajiwa kuwasilisha notisi katika majengo ya bunge. Waziri huyo mwenye ushawishi mkubwa serikalini alituhumiwa kwa kukiuka Sura ya Sita ya Katiba inayohusu uongozi na uadilifu.

"Ninapendekeza kutimuliwa kwa Waziri wa Masuala ya Ndani kwa misingi kwamba: (1) Amekiuka kifungu cha 73 cha Katiba kinachogusia uongozi na uadilifu; Ameshindwa kukomesha mauaji ya kiholela humu nchini na kuwatetea polisi kila mara wanapotuhumiwa kwa mauaji hayo," sehemu ya mswada huo ulisema.

Misingi mingine iliyotolewa ya kumtimua wazi huyo ni pamoja na kuleta mianya kati ya mamlaka ya bunge na ile ya ofisi ya rais.

Kwa kutia saini mswada huo, wabunge hao 92 wanaonekana kuunga mkono kutimuliwa kwa waziri huyo. Ilani hiyo sasa itasuburia Spika wa Bunge la Kitaifa ili Justin Muturi aliidhinishe.

Mnamo Juni mwaka uliopita, Ali alipata pigo baada ya Muturi kudinda kuidhinisha ilani aliyowasilisha ya kumtimua Waziri wa Uchukuzi James Macharia. Ali alikuwa amemwadikia Muturi akionyesha nia ya kuanzisha mchakato wa kumngo'a mamlakani waziri huyo kufuatia agizo lilitolewa kwamba kago zote zingepaswa kusafirishwa kupitia reli mpya ya SGR.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke