Naibu Spika wa Bunge la Uganda Anitah Among amewaelekeza wabunge kuwasilisha vyeti vya chanjo ya COVID-19 kabla ya kuingia bungeni.
Agizo hilo lililowataka wabunge hao kuwasilisha kadi zao za chanjo wakiingia bungeni lilitolewa Alhamisi, Oktoba 28Wabunge wa Uganda ni miongoni mwa watu wa kwanza Afrika Mashariki kupokea awamu ya kwanza na ya pili ya chanjo hiyo Mashirika kadhaa ya serikali yaliwaelekeza wafanyakazi wao pamoja na wageni kuwasilisha vyeti vya kabla ya kuingia ndani ya ofisi
Agizo hilo la kuwashurutisha wabunge kuwasilisha kadi zao wanapoingia bungeni, ulitolewa mnamo Alhamisi 28. Agizo hilo pia linatarajiwa kutekelezwa kuanzia wiki ijayo. Hatua hiyo ililenga kuwahimiza Waganda kupokea chanjo kwa kuwapa mfano mzuri kupitia wabunge wao.
"Kuanzia wiki ijayo, wabunge wote wanatakikana kuwasilisha cheti chao cha chanjo ya COVID-19 watakapoingia bungeni. Lazima tuwaonyeshe wananchi kwamba, sisi ni mfano mzuri kote nchini," Among alisema.