Makundi ya watu wanaotaka kujitenga yenye wafuasi wengi wa Tuareg nchini Mali, yamedai kuwaua takriban wanajeshi mia moja katika shambulio lililotokea katikati mwa nchi hiyo inayokumbwa na mzozo.
Taarifa kutoka kwa Mfumo Maalum unaongozwa na Uratibu wa Harakati za Azawad (CMA), muungano wa vikundi vilivyojitenga vya Tuareg ulisema kuwa wamelisababishia hasara kubwa jeshi - ikiwa ni pamoja na kujeruhi makumi ya askari, kuchukuliwa wafungwa watano, huku wakipoteza. saba kati ya wapiganaji wao wenyewe.
Madai yaliyotolewa na waasi hayakuweza kuthibitishwa kikamilifu. Maeneo ya matukio ni ya mbali na ni vigumu kupata vyanzo huru.
Operesheni hiyo inasemekana ilianza kwa shambulio la kujitoa mhanga, ambapo mhusika aliuawa, na kufuatiwa na shambulio la silaha nzito na nyepesi, inasema GSIM.
Kundi hilo pia lilidai kuua askari wengi na kudhibiti wadhifa huo na kuuchoma moto na kukamata magari sita na silaha na risasi nyingi.
Kaskazini mwa Mali kumeshuhudia kuongezeka kwa uhasama na CMA, ongezeko ambalo limendana na kujiondoa kwa ujumbe wa Umoja wa Mataifa, unalazimishwa kuondoka nchini na utawala wa kijeshi uliongia madarakani tangu 2020.
Tayari utawala wa kijeshi umewaamuru wanajeshi wa Ufaransa waliokuwa wakikabiliana na makundi ya jihadi kuondoka nchini humo tangu mwaka 2022.