Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Waasi wa Tuareg wadai kuwaua wapiganaji wa Wagner Mali

Marekani Yasema Haihusiki Na Mauaji Ya Madaktari Wa Cuba, Somalia Waasi wa Tuareg wadai kuwaua wapiganaji wa Wagner Mali

Fri, 2 Aug 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Waasi wanaotaka kujitenga kaskazini mwa Mali wamesema waliwaua mwishoni mwa mwezi Julai, makumi ya wapiganaji kutoka kundi la mamluki la Urusi la Wagner.

Zoezi hilo lilijumisha wanajeshi wa serikali karibu na mpaka wa Algeria. Waasi hao wanaotaka kujitenga wakiongozwa na jamii ya Tuareg wamesema hapo jana kwamba waliwaua wapiganaji 84 wa Wagner na wanajeshi 47 wa Mali katika siku tatu za mapigano makali yaliyoanza Julai 25 katika kambi ya kijeshi huko Tinzaouatene.

Kundi lenye mafungamano na Al-Qaeda la Jama'at Nusrat al-Islam wal Muslimeen (JNIM) pia lilidai kuwa lilishambulia msafara wa jeshi la Mali na washirika wake wa Wagner kusini mwa Tinzaouatene. Wachambuzi wamesema mashambulizi hayo yamekuwa pigo kubwa kwa mamluki wa Wagner barani Afrika.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live