Wafuasi wa Serikali ya mpito ya Sudan wamefanya maandamano katika barabara za mji Mkuu wa nchi hiyo wa Khartoum wakishinikiza kurejeshwa kwa utawala wa kijeshi.
Hata hivyo inaelezwa kuwa pande zote mbili za jeshi na Serikali ya mpito zimewataka wafuasi hao kuwa watulivu licha ya vikosi vya Polisi kuzidisha mashambulizi kwa waandamanaji hao.
Pande hizo mbili zinapingana na vikosi vya uhuru na mabadiliko, hasa kundi la Civilian Umbrella lililoongoza maandamano ya kitaifa yaliyompindua Rais Omar al- Bashir mwaka 2019.
Kundi hilo la Civilian linapingana vikali na wafuasi wanaoshinikiza Jeshi kuchukua mamlaka tena kuongoza nchi hiyo.