Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Waandamanaji wanaounga mkono Palestina wazuiliwa kwa muda Kenya

Waandamanaji Wanaounga Mkono Palestina Wazuiliwa Kwa Muda Kenya Waandamanaji wanaounga mkono Palestina wazuiliwa kwa muda Kenya

Mon, 23 Oct 2023 Chanzo: Bbc

Polisi wa Kenya wamewaachilia watu watatu waliokamatwa kwa kushiriki katika mkutano wa kuiunga mkono Palestina katika mji mkuu, Nairobi.

Watatu hao waliachiliwa Jumapili bila kufunguliwa mashtaka baada ya ukosoaji mkubwa kutoka kwa baadhi ya Wakenya, wanasiasa na mashirika ya kutetea haki za binadamu.Walisema walikuwa wakifanya "mkutano wa mshikamano".

Mbunge wa Kenya Yusuf Hassan alishtumu kukamatwa kwa watu hao.

Mkuu wa Amnesty International nchini Kenya, Irũngũ Houghton, alisema kuwa kuvurugwa kwa mkutano huo ni "kinyume cha sheria" na "kusumbua sana".

Ilikuwa imeandaliwa na Kamati ya Mshikamano wa Palestina ya Kenya baada ya polisi kusitisha maandamano ya awali ambayo kundi hilo lilikuwa limepanga nje ya ubalozi wa Marekani.

Rais William Ruto ameeleza kuunga mkono kikamilifu serikali yake kwa Israel katika mzozo unaoendelea.

Chanzo: Bbc