Wed, 15 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baadhi ya wafuasi wa Azimio wameshiriki katika maandamano yaliyofanyika katika Mji wa Kisumu wakipinga gharama ya maisha kuwa juu na kushinikiza Serikali ya Rais William Ruto kuchukua hatua.
Baadhi yao wakiwa wakiwa na masufuria, miko mabango yaliyoandikwa ‘Njaaaa!’ huku wakisikika wakiimba “Watu wa Kaunti ya Kisumu tumejitokeza kufanya maandamano kwa sababu Baba (Raila Odinga) alisema tufanye maandamano hadi Ikulu.”
Baadhi ya waandamanaji hao wamesema Machi 20, 2023 watashiriki katika maandamano makubwa zaidi yatakayofanyika Jijini Nairobi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live