Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

WFP: Uhaba wa chakula ni mkubwa Sudan

Sudan Wakimbizi Wakimbizi.jpeg WFP: Uhaba wa chakula ni mkubwa Sudan

Thu, 14 Dec 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limeonya siku ya Jumatano kuhusu "janga la chakula" linaloingoja Sudan ikiwa itashindwa kusambaza msaada muhimu wa chakula kwa watu waliokwama katika vita hivyo vilivyoikumba nchi hiyo kwa muda wa miezi minane.

"Ikiwa msaada wa chakula kwa watu waliokwama katika maeneo ambayo mapigano ni makali zaidi, mji mkuu Khartoum, Darfur (magharibi) na Kordofan (kusini), hautaongezeka kwa kiasi kikubwa katika kipindi kinachotangulia mavuno mwezi wa Mei, maeneo haya yanaweza kukumbwa na janga baya ya maafa ya chakula,” WFP imeonya katika taarifa yake.

Mnamo Aprili 15, mkuu wa jeshi, Jenerali Abdel Fattah al-Burhane na naibu wake, Jenerali Mohamed Hamdane Daglo, Mkuu wa Kikosi cha wanamgambo kinachoogopwa sana (FSR), walitafautiana.

Miezi hii minane ya vita imesababisha vifo vya watu 12,000 kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa. Kutokana na kukosekana kwa mavuno ya kuridhisha na kutokana na kuhama kwa watu kutokana na vita - watu milioni saba waliokimbia makazi yao wamerekodiwa na Umoja wa Mataifa - njaa inatishia kuangamiza sehemu zote za nchi.

Njaa "janga" kuna hatari ikumbe majimbo ya Darfur, ambapo Umoja wa Mataifa unashuku "mauaji ya halaiki", na kwa yale ya Kordofan, eneo lingine ambalo mapigano ni makali lakini pia mji mkuu, Khartoum, ambapo risasi za kwanza zilisikika Aprili. 15, ambao bado haufikiki huku mamilioni ya wakaazi bado wamenkwama.

Idadi ya Wasudan wanaokabiliwa na "njaa kali imeongezeka zaidi ya mara mbili katika mwaka mmoja", na kufikia "watu milioni 18", linaonya WFP. Nchi hiyo, ambayo iliwahi kuchukuliwa kama "kikapu cha mkate katika Afŕika Mashaŕiki,” iliŕikodiwa, kulingana na utafiti wa hivi majuzi wa WFP, "viwango vya juu zaidi vya njaa vilivyorekodiwa wakati wa msimu wa mavuno (Oktoba hadi Februari), kwa kawaida kipindi ambacho chakula kingi kinapatikana.

Wanajeshi hao walitangaza kwamba wamechukua "udhibiti kamili" wa El Daein, mji mkuu wa Darfur Mashariki, na kuashiria maendeleo ya hivi punde zaidi ya RSF huko Darfur.

Siku ya Jumapili, mkuu wa operesheni za kibinadamu za Umoja wa Mataifa nchini Sudan alitoa hofu kuhusu hatma ya Wasudan milioni 20 kati ya takriban milioni 48, au zaidi ya asilimia 40 ya watu, ambao shirika lake halina uwezo wa kuwafikia, na kuonya kwamba misaada ya kibinadamu. inaweza kukoma kutokana na ukosefu wa fedha.

"Pande zote katika mzozo lazima ziruhusu kusitishwa kwa misaada ya kibinadamu na kuhakikisha upatikanaji usiozuiliwa (wa misaada) ili kuepuka janga," Eddie Rowe, mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) nchini Sudan, alionya siku ya Alhamisi. Lakini kuzileta pande zote mbili kwenye meza ya mazungumzo bado ni lengo ambalo liko mbali.

Kwa ombi la mamlaka ya Sudan, Baraza la Usalama lilimaliza tarehe 1 Desemba kwa ujumbe wa kisiasa wa Umoja wa Mataifa ambao ulirekodi ukiukwaji wa haki za binadamu ambao umeongezeka tangu kuanza kwa vita

Chanzo: www.tanzaniaweb.live