Tue, 27 Feb 2024
Chanzo: Bbc
Vyama vya wafanyikazi nchini Nigeria vimeananza mgomo wa siku mbili Jumanne dhidi ya kuongezeka kwa gharama ya maisha.
Mfumuko wa bei katika uchumi mkubwa zaidi barani Afrika uko karibu 30% wakati sarafu ya ndani, naira, inashuka kwa kasi.
Uhaba wa umeme unazidisha ugumu wa maisha.
Benki ya Maendeleo ya Afrika imeonya kwamba hali ni tayari kwa machafuko ya kijamii.
Serikali inasema itapunguza matumizi ya umma na imeahidi hatua za kusaidia kaya na wafanyabiashara wadogo.
aijabainika ni wafanyikazi wangapi watashiriki migomo huku wengi wakishutumu vyama vya wafanyakazi kwa ufisadi.
Chanzo: Bbc