Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Virusi hatari kutoka India vya COVID-19 vyarekodiwa Kenya

07d147355b5c0ab4 Virusi hatari kutoka India vya COVID-19 vyarekodiwa Kenya

Wed, 5 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Yanayojiri kwa sasa ni kwamba aina hatari ya virusi vya COVID-19 vilivyogunduliwa nchini India, vimerekodiwa Kenya siku hii Jumatano Mei 5, 2021.

Kwa mujibu wa wizara ya Afya, visa vitano vinadaiwa kuripotiwa kaunti ya Kisumu na ni mara kumi na tano hatari zaidi kuliko virusi vilivyorekodiwa awali ulimwenguni.

Aidha, watu wengine 489 wamepatikana na virusi vya COVID-19 baada ya sampo 4, 426 kufanyiwa vipimo chini ya saa 24 zilizopita.

Akihotubia taifa, Katibu katika Wizara ya Afya Rashid Aman alisema kwamba idadi ya maambukizi kwa sasa nchini imefikia asilimia 11%, hii ikiwa ni asilimia mara dufu ikilinganishwa na ile iliyoripotiwa Jumanne, Mei 4.

Kati ya visa vilivyoripotiwa, 449 ni Wakenya ilhali 40 ni raia wa kigeni, kijinsia, 266 ni wanaume na 223 ni wanawake. Mgonjwa mdogo ana umri wa miezi minne na mkubwa ana miaka 102.

Kufikia sasa, idadi kamili ya maambukizi sasa imegonga 161,393kote nchini.

Habari za kuhuzunisha ni kwamba watu wengine 20 wamepoteza maisha yao kutokana na virusi hivyo, kwa jumla vifo vilivyorekodiwa nchini ni 2,825.

Wagonjwa 153 wamo katika vyumba vya ICU kati yao 28 wamewekwa kwenye ventilete na 111 wako kwenye wodi, 26 wanaangaaliwa wakipata nafuu.

India sasa inashuhudia wimbi kali la msambao wa virusi vya COVID-19 ambapo mataifa kadhaa yamesitisha safari za ndege kuelekea nchini humo, Tanzania ikiwa mojawapo.

Kuanzia Jumanne, Mei 4, kampuni ya ndege ya Tanzania, Air Tanzania ilitangaza kwamba imesitiasha safari zake hadi Mumbai, India hadi hapo itakapotoa taarifa nyingine ya kurudisha safari hizo.

Imeripotiwa kwamba mahospitali nchini India yamejaa wagonjwa na baadhi yao wamekuwa wakipoteza maisha yao wakiwa manyumbani kutokana na virusi hivyo.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke