Thu, 31 Aug 2023
Chanzo: Voa
Maafisa wa jeshi walionyakua mamlaka katika mapinduzi nchini Gabon siku ya Jumatano wamemtaja Jenerali Brice Oligui Nguema kuwa kiongozi wa mpito wa taifa hilo la Afrika Magharibi.
Jenerali Nguema hapo awali alibebwa kwa ushindi katika mitaa ya mji mkuu Libreville na wanajeshi wake.
Rais aliyeachishwa madaraka, Ali Bongo, ameonekana kwenye video akiwa nyumbani kwake, akitoa wito kwa “marafiki zake duniani kote” “wapige kelele” kwa niaba yake.
Koloni la zamani la Ufaransa ni mojawapo ya wazalishaji wakuu wa mafuta barani Afrika.
Chanzo: Voa