Viongozi kutoka mataifa ya Afrika Mashariki ya Shirikisho la Maendeleo la Pembe ya Afrika IGAD, wamemtaka Rais wa Sudani Kusini, Salva Kiir kumaliza mgogoro baina ya tafa hilo na Ethiopia.
Umoja huo umesisitiza jambo hilo kupitia Waziri Mkuu wa nchini humo, Abdallah Hamko,na kutaka afikishe suala hilo kwa Rais kwani ndiye mtu sahihi wa kumaliza sintofahamu hiyo.
"Mwenyekiti wa IGAD, ameomba Rais kiir aende nchini Ethiopia kwa kuwa wana amini ndiye mtu sahihi ambaye anaweza kutatua mgogoro huu, hata hivyo wamesisitiza zaidi kwani wana amini anaweza kumudu maongezi baina ya pande zote mbili"Amesema Waziri huyo.
Hata hivyo, taarifa zaidi zinaeleza kuwa tayari Ofisi ya Rais imeshapokea ombi hilo na imekubali kulifanyia kazi kwa haraka.