Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Viongozi Haiti wakalia kuti kavu...

Haiti Inaafiki Jeshi La Kimataifa Linaloongozwa Na Kenya Viongozi Haiti wakalia kuti kavu...

Fri, 20 Oct 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilirejelea upya siku ya Alhamisi, Oktoba 19, vikwazo dhidi ya viongozi kadhaa na vikwazo vya silaha ndogo ndogo nchini Haiti kwa mwaka mmoja, lakini bila kuzingatia ufichuzi wa "milipuko" wa jopo la wataalamu wake na bila kuongeza majina kwenye orodha ya waliochukuiwa vikwazo.

Kwa mwaka mmoja, jina moja tu kwenye orodha hii, lile la afisa wa polisi wa zamani ambaye alikua kiongozi mashuhuri wa muungano wa genge, Jimmy Chérizier, aliyepewa jina la utani la Barbeque. Analengwa na vikwazo vya kuzuiwa kwa mali na marufuku ya kusafiri. Bado, jopo la majaji lilipendekeza kuwawekea vikwazo watu zaidi wanaoaminika kuwa na uhusiano na magenge na ni watu mashuhuri wa kisiasa na kiuchumi nchini Haiti.

Baada ya ziara yake na uchunguzi wake, jopo la wataalam waliorodhesha watu wenye ushawishi mkubwa walio na uhusiano na makundi ya magenge ncini Haiti, ambayo yanazua machafuko nchini na kudhibiti 80% ya Port-au-Prince. Majina yao yametangazwa kwa umma, anaripoti mwandishi wetu wa New York, Carrie Nooten.

Miongoni mwa malengo ya ripoti hiyo, watu wanne wanaojulikana sana wanashutumiwa kuwa na silaha au kutumia magenge: rais wa zamani Michel Martelly mwenyewe, kwanza ya yote: kulingana na jopo la Umoja wa Mataifa, alitumia magenge haya yenye silaha kupanua ushawishi wake wa muhula wake, kati ya mwaka 2011 na 2016.

Wengine wanaolengwa ni seneta wa zamani na kiongozi wa Bunge la Seneti Youri Latortue, kiongozi wa chama cha Prophane Victor na mfanyabiashara mashuhuri Reybold Deeb. Waziri Mkuu wa zamani wa Michel Martelly, Laurent Lamothe, anashutumiwa kwa ubadhirifu wa mamilioni ya dola za pesa za umma zilizokusudiwa kwa waathiriwa wa tetemeko la ardhi. "Hofu iliyoenea" ya magenge

Hata hivyo, baadhi ya wajumbe wa Baraza hilo hadi sasa wamekataa kuwaongeza kwenye orodha ya waliowekewa vikwazo kwa madai kuwa hawakuwa na muda wa kutosha wa kuhakiki taarifa hizo. China, Brazil na Marekani zilisisitiza kwamba majina haya yaongezwe.

Mnamo Oktoba 2, Baraza la Usalama liliidhinisha kutuma ujumbe wa kimataifa nchini Haiti unaoongozwa na Kenya kusaidia polisi waliozidiwa na magenge, "mwale wa matumaini" kulingana na nchi hii maskini ya Caribbean, ambapo rais Jovenel Moïse aliuawa majira ya joto ya 2021 Ubakaji kutumika kama silaha za ugaidi

Watu kuchomwa moto wakiwa hai, utekaji nyara kwa ajili ya fidia... Wakati ghasia za magenge yanayodhibiti sehemu kubwa ya mji mkuu wa Port-au-Prince zikiendelea kuwa mbaya, Waziri Mkuu Ariel Henry na Umoja wa Mataifa. Katibu Mkuu Antonio Guterres amekuwa akitoa wito kwa ujumbe wa msaada wa polisi tangu Oktoba 2022.

Mnamo Oktoba 11, katika mahojiano na shirika la habari la AFP, mkurugenzi wa polisi wa eneo hilo Frantz Elbé alionyesha matumaini kwamba jeshi hili la kimataifa litasaidia idara yake kupigana dhidi ya "ugaidi wa magenge uliokithiri".

Chanzo: www.tanzaniaweb.live