Viongozi wa mataifa saba yanayounda Jumuiya ya Afrika Mashariki wanatarajiwa kukutana kujadili hali ya usalama katika eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kulingana na taarifa ya serikali.
Viongozi hao wanakutana kwa mualiko wa mwenyeji wao Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ambaye pia ni mwenyekiti wa Jumuiya hiyo.
Muda mfupi uliopita Rais wa Uganda Yoweri Museveni amethibitisha kwenye mtandao wake rasmi wa Twitter kwamba amewasili jijini Nairobi kkuhudhuria Kikao cha Tatu cha Wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
I have arrived in Nairobi, Kenya for the 3rd East African Community (EAC) Heads of State Conclave on the peace and security situation in the Democratic Republic of Congo (DRC). pic.twitter.com/3XNXcGcejB
— Yoweri K Museveni (@KagutaMuseveni) June 20, 2022