Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Viongozi 6 wa Afrika kutatua mgogoro wa Ukraine na Urusi

Ukraine Yadai Kukomboa Maeneo Bakhmut Baada Ya Urusi Kukanusha Viongozi 6 wa Afrika kutatua mgogoro wa Ukraine na Urusi

Tue, 23 May 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Ujumbe wa viongozi hao wa nchi 6 za Afrika unatarajiwa kufanya mazungumzo na pande mbili wenye lengo la "kuanzisha mchakato wa amani."

Rais wa Urusi, Vladimir Putin na Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelenskyy wote wamekubali kuwa wenyeji wa ujumbe huo kutoka Afrika Kusini, Senegal, Misri, Jamhuri ya Congo, Uganda na Zambia.

Mazungumzo hayo pia yanaungwa mkono na Marekani, Umoja wa Ulaya, Umoja wa Mataifa, Umoja wa Afrika na China.

Ukraine inataka Urusi iondoe majeshi yake katika ardhi yake wakati Urusi yenyewe inashinikiza Ukraine ikubali kuliachia eneo la Crimea.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live