Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Vifo 3 vyaripotiwa huku watu wengine 796 wakipatikana na virusi vya COVID-19

183258bf2a43c9f9 Vifo 3 vyaripotiwa huku watu wengine 796 wakipatikana na virusi vya COVID-19

Fri, 18 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Wizara ya afya imetangaza kwamba watu wengine 796 wamepatikana na virusi vya COVID-19 baada ya sampo 7,392 kufanyiwa vipimo chini ya saa 24 zilizopita.

Kufikia sasa nchi imerekodi visa 178, 078 huku asilimia ya maambukizi ikifikia 10.8%

Kati ya visa hivyo, 746 ni Wakenya ilihali 50 ni raia wa nchi za kigeni.

Watu wengine 328 wamepona kutokana na virusi hivyo, 307 walikuwa chini ya utunzi wa nyumbani ilhali 21 walikuwa wakipokea matibabu katika hospitali mbali mbali.

Kwa jumla idadi ya watu waliopona nchini imefikia 122,346.

Wizara ya Afya pia imetangaza kwamba watu wengine watatu wamefariki dunia kutokana na ugonjwa huo, jumla ya vifo vilivyoripotiwa nchini kwa sasa ni 3,437.

Wagonjwa 1, 097 wamelazwa katika hospitali mbali mbali ilhali 4,842 wako chini ya utunzi wa kimatibabu nyumbani.

Kulingana na wizara ya afya, wagonjwa wengine 89 wamelazwa katika vyumba vya wagonjwa mahututi, 26 wamewekwa kwenye ventileta, 49 kwenye oksjeni na 14 wanachunguza.

Kaunti ya Nairobi bado inaongoz kwa idadi ya maambukizi ikiwa na visa 174, Siaya 138, Kisumu 92, Bomet 62, Mombasa 46, Busia 41, Homa Bay 30, Kisii na Uasin Gishu vikiwa na visa 24 kila moja

Nayo kaunti ya Vihiga imerekodi visa 23, Kakamega 19, Nakuru 16, Trans Nzoia 15, Bungoma 13, Kilifi 11, Kiambu 9, Kajiado, Kericho na Meru visa vinane kila moja, Nandi 6, Garissa na Kwale 4 na Migori visa vitatu.

Haya yanajiri baada ya erikali kutangaza kafyu ya kutokuwa nje kati ya saa moja jioni hadi saa kumi asubuhi katika kaunti za eneo la Nyanza.

Hii ni kufuatia ongezeko la maambukizi ya virusi vya COVID-19 eneo hilo.

Kaunti zitakazo athirika ni Vihiga, Busia, Kisii, Nyamira, Kakamega, Kericho, Bomet, Bungoma, Trans-Nzoia, Kisumu, Homa-Bay, Siaya, na Migori.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke