Dar es Salaam. Baadhi ya Watanzania wanaoishi Afrika Kusini, Uganda na Kenya wamezungumzia jinsi wanavyoishi baada ya shughuli mbalimbali nchini humo kusimamishwa, na baadhi wananchi kuzuiwa kutoka nje.
Mathalani Afrika Kusini wananchi wamezuiwa kutoka nje kuanzia jana, huku Kenya wakitakiwa kukaa ndani kuanzia saa 1 jioni.
Wakizungumza na Mwananchi Digital wameeleza changamoto wanayokumbana nayo kwa kukaa ndani ili kuepuka maambukizi zaidi.
Machi 24, 2020 Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa alitangaza zuio la watu kutoka nje huku Machi 27, 2020 Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta akipiga marufuku wananchi kutembea kuanzia saa 1 jioni.