Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Utata kuhusu nakala feki za BBI waendelea huku IEBC ikijitenga na lawama

F2a4898a92cadbe2 Utata kuhusu nakala feki za BBI waendelea huku IEBC ikijitenga na lawama

Fri, 23 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Mwenyekiti wa tume hiyo Wafula Chebakati alisema IEBC kwanza alipokea nakala sita zilizochapishwa za rasimu ya Mswada wa BBI 2020 mnamo Desemba 2020

- IEBC baadaye iliitisha nakala zingine zilizochapishwa, na ilipokea 57 na kutuma nakala 47 kwa mabunge ya kaunti mnamo Januari 2021

- Iliibuka kuwa mabunge 34 ya kaunti yalishughulikia mswada uliokuwa na makosa ambao uliorejelea kifungu kisichokuwepo cha katiba

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) imefafanua kwamba iliwasilisha nakala za mswada wa Mchakato wa Maridhiano (BBI) ilivyopokea kutoka kwa wanaouunga mkono.

Mwenyekiti wa tume hiyo Wafula Chebakati alisema tume yake kwanza ilipokea nakala sita zilizochapishwa za rasimu ya Mswada wa Marekebisho ya Katiba 2020 mnamo Desemba 10, 2020.

Baada ya kuthibitisha maelezo kuwahusu wanaounga mkono, mnamo Januari 26, 2021, IEBC iliwaomba waungaji mkono wa BBI nakala za ziada zilizochapishwa, na ilipokea 57 na kuzituma nakala 47 kwa mabunge ya kaunti.

"Siku hiyo hiyo, wahamasishaji kuhusu BBI waliwasilisha kwa tume nakala 57 za Mswada huo, ambapo tume hiyo iliwasilisha nakala 47 kwa mabunge ya kaunti," Chebukati alisema.

Hali hii ilijiri wakati kukiwa na madai kwamba mchakato wa BBI unaweza kukumbana na kikwazo baada ya vyombo mbalimbali vya habari kuripoti kwamba mabunge ya kaunti kadhaa yalipitisha mswada huo kwa kutumia matoleo tofauti.

Ilibainika kuwa mabunge 34 ya kaunti yalishughulikia mswada wenye makosa ambao ulitaja kifungu cha katiba ambacho hakipo wakati ukielezea jinsi maeneo 70 yangeundwa.

Hiyo ilimaanisha bunge pia lilipokea matoleo tofauti, na hali hii imeiweka Kamati ya Pamoja iliyoshughulikia ripoti ya mwisho itakayowasilishwa katika Bunge wiki ijayo katika hali ya kuchanganyikiwa.

HujumaKatibu wa Sekretarieti ya BBI Paul Mwangi alisema hawajui kilichotokea kwani waraka huo ulipotumwa moja kwa moja kwa IEBC.

"Mswada umepelekwa moja kwa moja kutoka IEBC hadi mabunge ya kaunti. Haya yanayotokea sasa ni njama ya kutatiza mchakato kupitia mahakama. Watu wanatafuta tu sababu za kukwamisha BBI kwa sababu wameshindwa kisiasa," alisema Mwangi Jumatano, Aprili 21.

Kulingana na Kamati ya Pamoja ya Haki na Sheria ya Bunge, ni mabunge 13 tu kati ya 47 ya kaunti yaliyokuwa na toleo sahihi la ripoti hiyo.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke