Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Utata: Mwanafunzi Akutwa Amefariki Hostel

Video Archive
Sun, 7 Nov 2021 Chanzo: globalpublishers.co.tz

Familia moja mjini Kisii Nchini Kenya imeziomba mamlaka za uchunguzi kubaini kilichomuua mtoto wao wa kiume aliyekutwa amefariki kwenye kitanda chake ndani ya bweni lao shule yao.

Taarifa zinaeleza kuwa marehemu Enock Morara ambaye alikuwa mwanafunzi wa kidato cha nne katika Shule ya Upili ya St.Paul Amasago eneo la Keumbu, kaunti ya Kisii alilala kama kawaida lakini hakuamka kama wenzake walivyoamka na baadaye akagundulika amefariki.

Uchunguzi wa kitabibu uliofanyika katika hospitali ya Rufaa ya Kisii bado haujabaini chanzo cha kifo cha mtoto huyo.

Wakati huo huo, maofisa wa Polisi nao wanaendelea na uchunguzi zaidi kuhusu kifo cha mwanafunzi huyo.

Na Innocent Matara – Global TV Kenya

Chanzo: globalpublishers.co.tz