Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Usalama wa DP Ruto: Raia wa Kigeni Akamatwa Baada ya Kurusha Drone Karen

08b30490f99099f2 Usalama wa DP Ruto: Raia wa Kigeni Akamatwa Baada ya Kurusha Drone Karen

Tue, 30 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Mama Rachael Ruto alikuwa nyumbani wakati aligutushwa na kifaa kilichokuwa kikizunguka angani

- Aliwasiliana na maafisa wa polisi ambao walifika kuchunguza kilichokuwa kikiendelea na ndipo raia wa kigeni akatiwa mbaroni

- Amekuwa akihojiwa kuhusiana na kisa hicho ambacho kilizua maswali kuhusu usalama wa DP

- Wandani wa DP wamekuwa wakiteta kuwa polisi wamekuwa wakipuuza usalama wa DP

Polisi wamemtia mbaroni raia mmoja wa kigeni baada ya kurusha drone aliyokuwa akipeperusha nyumbani kwa Naibu Rais William Ruto Karen.

Kamanda wa polisi kaunti ya Nairobi Augustine Nthumbi alidhibitisha kisa hicho akisema tukio hilo lilifanyika Jumatatu Machi 29.

Rais huyo wa kigeni ametambulika kama Hind Jeremy na maafisa wa polisi walimzuilia ili kumhoji kuhusiana na yaliyotokea.

Duru za polisi zilisema tukio hilo lilichukuliwa kwa uzito kwani ni tishio kwa usalama wa Naibu Rais.

Mama Rachael Ruto ndiye aliripoti kisa hicho kwa polisi baada ya kuona kifaa hicho kilichokuwa kikizunguka boma lao kutoka hewani.

Makachero walijihami na kukimbia Karen ambapo walifahamu ilikuwa ni drone kutoka boma la jirani wa Ruto.

Na kuchukua hatua ya kwanza ya kumhoji kuhusiana na kilichokuwa kikiendelea hadi kifaa chake kufika kwa DP.



Wandani wa DP wamekuwa wakiteta kuhusu usalama wake wakidai polisi wamepokea maagizo kutoshika doria ipasavyo.

Wabunge 100 wanaoegemea upande wa Naibu Rais William Ruto tarehe nane Februari walimwandikia barua inspekta mkuu wa polisi Hillary Mutyambai wakilalamika kuhusu usalama wa DP.

Msemaji wa polisi Charles Owino hata hivyo alikanusha madai hayo akisema DP ni mojawapo wa watu wanaolindwa vikali. Alisema yeye hulindwa na walinzi kutoka vitengo vitatu ili kuhakikisha hakuna hata mbu ambaye anamguza kiongozi huyo.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari kemkem za TUKO

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke