Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Usaidizi wa Rais Uhuru Wamgusa Kimani Ngunjiri, Asema Sasa Amebadilika

F0ce43284800d664 Usaidizi wa Rais Uhuru Wamgusa Kimani Ngunjiri, Asema Sasa Amebadilika

Fri, 26 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Ngunjiri amekuwa akimshambulia Rais Uhuru kutokana na tofauti zake za kisiasa na DP Ruto

- Licha ya hilo Rais alikuwa mmoja wa wale ambao walitoa mchango mkubwa kusaidia familia ya Ngunjiri kulipa bili ya hospitali ya mwanawe

- Anasema hilo ni funzo kubwa maishani kuwa unaowadhani kuwa mahasimu huenda ndio marafiki wakuu

Mbunge wa Bahati Kimani Ngunjiri amesema amebadilika na atakuwa askofu wa kueneza amani baada ya funzo alilopata alipompoteza mwanawe.

Ngunjiri alisema aliokuwa akiwaona kama mahasimu wake ndio walikuwa na usaidizi mkubwa kipindi hicho kigumu kwa familia yake.

Arthur Kinyanjui alifariki mwezi Machi baada ya kuwa katika hospitali ya Agha Khan Mombasa tangu mwezi Disemba 2020.

"Wakati mwingine mambo magumu hufanyika ili kutupa funzo maishani. Kifo cha mtoto wangu AK kimenifunza mengi maishani. Wale ambao niliwaona kama mahasimu wangu ndio walikuwa wa kwanza kunipa bega la kulilia," alisema mbunge huyo.



Alisema alichokipitia kimembadilisha na sasa atakuwa akieneza injili ya amani na ataanzia nyumba ya Jubilee ambapo baba na mama wako na ugomvi.

"Nimeamuwa kuwa wakala wa kutafuta amani na nitaanza na ndugu yangu Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto. Naamini hakuna tofauti za kisiasa zisizo na suluhu na ninaamini kufikia mwishoni mwa mwaka Rais na naibu wake watakuwa wakifanya kazi pamoja kama ndugu," alisema Ngunjiri.

Mbunge huyo wa Bahati amekuwa mmoja wa wakosoaji wakuu wa Rais Uhuru tangu tofauti ziibuke ndani ya Jubilee na DP kuonekana kutengwa.



Licha ya kuwa akimtupia cheche kali Rais kupitia kwa vyombo vya habari, Uhuru alikuwa katika mstari wa mbele kumsaidia kulipa bili ya hospitali iliyoachwa na mwanao.

Kulingana na duru za kuaminika Rais alitoa mchango wa KSh 2M ili kulipia bili iliyoachwa na Arthur Kinyanjui.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke