Tue, 14 Sep 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiongozi wa upinzani nchini Guinea, Cellou Dalein Diallo ameutaka uongozi wa kijeshi nchini humo kuunda serikali ya mpito na kutangaza muda wa kufanyika uchaguzi
Diallo amesisitiza kuwa jeshi kwa sasa lazima lithibitishe nia yake ya kurejesha mamlaka kwa raia kama walivyoahidi wakati mapinduzi dhidi ya rais Alpha Conde Septemba 5.
Aidha amemshutumu rais Conde aliyeondolewa madarakani kwa kujiangamiza mwenyewe baada ya kuwa na fikra ya muhula wa tatu madarakani kwa kusema ukomo wa madaraka kikatiba hauna nafasi kwake.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live