Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Unakula pesa za umma bure, jiuzulu: Raila amwambia DP Ruto

D933cbb6c84f5b31 Unakula pesa za umma bure, jiuzulu: Raila amwambia DP Ruto

Fri, 27 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Raila alisema DP anafaa kuondoka serikalini kwani hana majukumu anayotekeleza kwa sasa baada ya majukumu yake kuchukuliwa na Waziri Fred Matiang'iAlimtaka awe mkakamavu na kufanya alichofanya mzee Jaramogi Oginga wakati wa utawala wa Kenyatta alipojiuzuluRuto amekuwa akisema ametengwa serikalini na Rais Uhuru Kenyatta tangu handisheki kufanyikaKinara wa ODM Raila Odinga amemtupia vijembe Naibu Rais William Ruto akisema anafanya kosa kuikashifu serikali.

Raila alisema DP Ruto hafai kuikosoa serikali akiwa angali anahudumu kama msaidizi wa Rais Uhuru Kenyatta.

Raila alisema Ruto anafaa kuwa na msimamo kisiasa na hivyo aondoke serikalini iwapo anahisi hakubaliana na mwelekeo wa Rais.

"Kama yuko na msimamo, angeondoka. Ajiuzulu, ukienda hata kwenye kumbukumbu utapata barua ya babangu aliposema hawezi kuendelea kupata mshahara bila majukumu," alisema Raila.

Alimtaka DP ajiuzulu mara moja akisema ni kosa kuendelea kupokea mshahara ilhali hana majukumu.

Raila alisema Ruto amekuwa mjanja kisiasa na sasa anajaribu kuhepa lawama za kufeli kwa serikali.



Read also

This Country Should Be Disbanded: Mfuasi Sugu wa Raila Akutana na Junet Mohammed

"Yeye sasa ameamua hataki kubeba msalaba wa mabaya ya serikali. Eti anasema mazuri tumefanya, lakini mabaya anasema eti ni Raila na Uhuru. Mimi siko katika serikali, hakuna mimi nimefanya kuzuia serikali kufanya kazi yake," alisema Raila.

Raila alitetea ushirikiano wako na Rais akisema handisheki ilisaidia kutuliza mzozo wa kisiasa nchini.



"Nchi ilikuwa inatumbukia kwenye mgogoro, na ndipo tukasalimiana na Uhuru. Lakini mimi siko serikalini. Hakuna mtu ya upande yangu ameajiriwa serikalini, nazuia serikali na nini?" aliongeza wakati wa mahojiano na redio zinazopeperusha kwa lugha ya mama.

Kuhusu siasa za 2022, Raila alisema anaendelea kushauriana na wandani wake ili afanye uamuzi wa iwapo atawania kiti cha urais.

"Bado nitaangalia, mimi nashauriana na ninaweza kufanya kazi na kila mtu kote nchini. Nitawania iwapo Wanjiku anataka niwanie," alisema.

Aliongeza kuwa bado hajaamua ni nani atakuwa mgombea mwenza wake kwenye kinyang'anyiro hicho.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690



Read also

Magazeti Jumanne, Agosti 24: Njaa Yawakeketa Wakenya Viongozi Wakishiba

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke