Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Unafaa kuwa jela, Raila amlipua DP Ruto wakati wa mazishi ya Kalembe

695567855f3fece5 Unafaa kuwa jela, Raila amlipua DP Ruto wakati wa mazishi ya Kalembe

Sat, 12 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Raila alisema Kalembe alikuwa hustler wa kweli na wala si kama vigogo wengi aliosema ni unafiki wanaoendeleza

- Alisema serikali yake itaziba pengo zote ili kuhakikisha hakuna mali ya umma ambao inaibwa na vigogo kujitayarisha

- Matamshi ya Raila ilikuwa wazi kuwa yanamlenga naibu rais William Ruto ambaye amekuwaakihudhuria michango kanisani

Kinara wa ODM Raila Odinga Ijumaa Juni 11 alifufua mashambulizi yake makali dhidi ya Naibu Rais William Ruto.

Wakati wa kumuomboleza mwanasiasa Kalembe Ndile, Raila alisema alikuwa mlala hoi wa kweli aliyejitahidi kufaulu maishani.

"Alikuwa mzalendo wa kweli wa Kenya. Alikuwa akipigania maisha ya watu wa chini kwa sababu yeye alitoka humo. Alikuwa hustler wa kweli," alisema Raila.

Raila alisema Kenya ina utajiri mkubwa lakini mali yake inaibwa na vigogo wachache uongozini.



Matamshi yake yalionekana kumlenga DP Ruto wazi haswa kutokana na hafla za kutoa misaada ambazo amekuwa akihudhuria kuinia makundi kwenye jamii na pia kujenga makanisa.

Lakini sasa kuna wanafiki ambao wamekaa pale wanaiba pesa, anakuja kwenu amebeba pesa zenu na kusema mniite kwa michango ya makundi ya vijana na kina mama. Pesa ambazo ameiba

Ni watu ambao wanafaa kuwa ndani ya jela lakini ni wanafiki tupu. Wanafaa wawe jela," aliongeza.

Alisema serikali yake italeta mfumo wa uongozi kama ulioanzishwa na aliyekuwa rais wa Tanzania John Magufuli akisema uliziba nafasi za wizi wa mali ya umma.

"Pesa inaibwa na wachache waliopewa jukumu na wananchi . . . tutaziba mwanaya na mtaona maendeleo inaanza kutendeka," alisema Baba.

Magufuli alijulikana kwa kukabiliana na mafisadi nchini mwake kwa makali ya chui mwenye hasira.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari kemkem za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke