Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Umoja wa Afrika kununua chanjo milioni 110 za Moderna

Bapic Umoja wa Afrika kununua chanjo milioni 110 za Moderna

Wed, 27 Oct 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Umoja wa Afrika (AU) unakusudia kununua dozi milioni 110 za chanjo ya COVID-19 kutoka Moderna Inc katika mpango ulioratibiwa kwa sehemu na Ikulu ya Marekani, White House.

Dozi hizo zitatolewa katika miezi ijayo, huku milioni 15 zikiwasili kabla ya mwisho wa 2021, milioni 35 katika robo ya kwanza ya mwaka ujao na hadi milioni 60 katika robo ya pili.

Kupitia barua pepe, mjumbe wa AU wa coronavirus Strive Masiyiwa alisema hatua hii ni muhimu kwani inaturuhusu kuongeza idadi ya chanjo zinazopatikana kwa haraka.

Hata hivyo, shehena hiyo ya chanjo ni chini ya idadi ambayo Afŕika inahitaji kuwachanja watu wake bilioni 1.3, ambao wamekuwa na upatikanaji mdogo sana wa chanjo kulinganisha na nchi zilizoendelea zaidi duniani.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live